VITABU VYA MWANDISHI.
Vitabu hivi ni adimu na havipatikani kwa urahisi kwani havijaenea kila mahali duniani. Ni neema ya pekee kuwa na nakala ya vitabu hivi, kwani vitakuwa msaada wa kiroho kwako binafsi ndugu, jamaa, majirani, marafiki, wapenzi, wafanyakazi, watumishi na wengineo utakaowiwa kuwapatia zawadi hii muhimu kwa ajili ya maisha ya ufalme wa Mungu. Mungu amekusudia kuwapa mafundisho haya kupitia mimi na wewe ili tuweze kuwafikia wengine kwa lugha zao na kwa kutumia njia mbalimbali za mawasiliano kama tepurekoda, santuri, mikanda ya video , Redio, Runinga, nakadhalika. Huduma hii ya kiroho ni ya kila asikiaye na kuamini .
1, Jinsi Mungu anavyoweza kunifunua kwa watu kwa njia (10) Hatua saba za kusikia sauti ya Mungu waziwazi-Live.Kimekuwa msaada kwa wengi kwani Mungu amejifunua na kusema nao moja kwa moja kwa kunyoosha mkono wake, kujibu maswali yao waliokuwa wakijiuliza yaliyohitaji majibu. Yawezekana kila mmoja wetu ana kiu na anahitaji kufunuliwa na kusema naye waziwazi. Jibu la kiu tulizonazo ni kupitia haya, atajibu haja zako ambazo huenda umeziomba kwa muda mrefu. Tumia hatua saba za matendo ili ajifunue kwako
2. Jifunze kusamehe na kusahau Mungu akukumbuke Kabla na Baada ya kufa na Akufunulie, “Mambo ambayo jicho halikuyaona wala sikio halikuyasikia, (Wala hayakuingia katika moyo wa mwanadamu). Mambo ambayo Mungu aliwaandalia wampendao”(1Kor.2:9)
Kitabu
hiki kimekuwa msaada kwa wengi kuondoa chuki kati yao na kuchochea upendo,
kubadili huzuni kuwa furaha, mauti kuwa uzima, uadui kuwa urafiki, uponyaji na
mambo sawa nayo (1Kor.2:9). Baada ya Yesu kujifunua na uungu wake kuthibitisha
neno. Ninaamini nawe ni zamu yako sasa upate ufunuo wa ajabu utakaokupelekea
kujisahihisha na kuwasamehe wengine. Kimekuwa msaada kwa ajili ya kanisa lake
pia, ili lisiwe na mawaa katika kueneza pendo lake na kumdhihirisha Mungu wa
mapendo.
3. Utoaji wa sadaka matoleo aina 7 unavyoweza kusababisha Mungu
Akukumbuke na Akufunulie, “Mambo ambayo jicho halikuyaona wala sikio
halikuyasikia, (Wala hayakuingia katika moyo wa mwanadamu). Mambo ambayo Mungu
aliwaandalia wampendao” (1Kor.2:9).
Kinaachilia ufunuo wa tafsiri za utoaji wa matoleo, kwani kutoa
ni zaidi ya fedha na mali, kukufunulia nguvu uungu, uweza uliositirika katika
kila aina ya matoleo au sadaka unayoachilia. Matoleo hufafanya mambo ambayo
huwezi kuyapata kwa njia nyingine yoyote ile. Hivyo jibu la hitaji lako
yawezekana limefichwa ndani ya matoleo ya aina mojawapo kati ya saba. Wenzetu
walipofunuliwa hayo yanayotaka ufahamu walikuwa wanatoa wakijua mbegu hiyo
ndani yake imebeba nini? Uungu wa mtoto, kuondoa utasa, ulinzi na Baraka.
4. Kanuni saba (7) za jinsi ya kutoa sadaka/ matoleo yako yapokelewe
mbinguni ili Mungu aweze kukujibu, Akukumbuke na Akufunulie… Kinajibu kwa nini wengi wanatoa (wanapanda mbegu) lakini
hawavuni?. Wakati mwingine wanakuwa makini kutoa kidogo au hudhubutu kutotoa.
Maana kwao hudhani kuwa ni njia ya
kupungukiwa na sio njia ya kuongeza mtaji, mafanikio, baraka na uungu. Utaelewa
jinsi ya kutoa kwa ukimya namna Mungu
anavyotaka na kama alivyofanya kwa wenzetu walivyokuwa wanaambatanisha maombi
yao na imani na matoleo atajibu; vivyo hivyo atatenda kwako. Kwa kuzingatia kanuni hizo saba (7)
mbingu hupokea matoleo yako.
KITABU
No comments:
Post a Comment